Mazingira FM

Mwenyekiti UVCCM Bunda awajibu wanaharakati wanaochochea vurugu

28 May 2025, 6:38 pm

Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Bunda ndugu Mohamed Juma Msafiri

Amewataka wananchi na wanachama wa chama hicho kuwa makini na watu wanaotoka nje ya nchi na kutaka kuleta vurugu na chokochoko hapa nchini.

Na Adelinus Banenwa

Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Bunda ndugu Mohamed Juma Msafiri amewataka wananchi na wanachama wa chama hicho kuwa makini na watu wanaotoka nje ya nchi na kutaka kuleta vurugu na chokochoko hapa nchini.

Mohamed ameyasema hayo katika mtaa wa Mcharo kata ya Mcharo halmashauri ya mji wa Bunda kwenye hafla ya kumpokea mwanachama mpya kutoka chama cha wananchi CUF ndugu Dustan ambaye pia alikuwa mgombea wa kiti cha udiwani wa kata hiyo kwa mwaka 2015 na 2020.

Baadhi ya wanachama na viongozi wa CCM kata ya Mcharo

Mohamed amewatahadharisha wanachama kuwa kumekuwepo na watu kutoka mataifa jirani wanaojiita wanaharakati lakini lengo lao likionekana ni kutaka kuvuruga amani ya nchi hivyo amewataka wananchi kutowaunga mkono.

Sauti ya Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Bunda ndugu Mohamed Juma Msafiri