Mazingira FM

Bunda: Grumeti Fund washiriki zoezi la amwani za makazi kwa kutoa vibao 31 vyenye thamani ya zaidi ya milion mbili

28 April 2022, 1:10 pm

Kampuni ya Grumeti Fund wameshiriki zoezi la anwani za makazi kwa kuchangia kuto vibao vya anwani za makazi 31 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi million mbili

Akizungumza katika makabidhiano hayo mwakirishi wa kampuni ya Grumeti Fund, Davidi Mwakipesile amesema wamechangia kwa lengo la kuunga mkono juhudi za serikali katika zoezi la anwani za makazi linaloendelea hapa nchini

DAVID MWAKIPESILE, AFISA UHUSIANO GRUMETI FUND – AKIKABIDHI VIBAO VYA ANWANI ZA MAKAZI

.

 

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bunda Mh Joshua Nassari Amewashukuru Grumeti kwa kuunga mkono zoezi la anwani za makazi zoezi ambalo linaendelea nchi nzima kwa sasa

.

Mh Nassar ameongeza kuwa vibao vilivyotolewa na Kampuni ya Grumeti vina kiwango

.

Hata hivyo ametoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo