Mazingira FM

Masaburi: urasimu chanzo kusitishwa mikopo ya halmashauri

16 July 2023, 12:28 pm

Mhe Juliana Didas Masaburi mbunge viti maalumu CCM kupitia kundi la vijana, Picha na Adelinus Banenwa

Urasimu chanzo cha kusitishwa kwa mikopo ya asilimia kumi kutoka mapato ya ndani ya halmashauri ambapo serikali inaandaa mfumo mwwingine ambao makundi ya akina mama vija na wenye ulemavu watatumia kupata fedha hizo.

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa serikali imeamua kubadirisha mfumo wa kukopesha vikundi katika mpango wa asilimia kumi kutoka mapato ya ndani ya halmashauri nchini kutokana na urasimu uliyokuwa unatumika katika mikopo hiyo.

Hayo yamesemwa na mbunge viti maalumu CCM kupitia kundi la vijana Mhe Juliana Didas Masaburi katika baraza lililoandaliwa na Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Bunda ambapo pamoja na mambo mengine alifika kusikiliza kero za vijana na changamoto ndani ya jumuiya hiyo.

Mhe Masaburi amesema kutokana na changamoto hiyo ya urasimu serikali imelazimika kubadirisha mfumo baada ya wabunge kuishauri hivyo kuanzia dirisha litakapofunguliwa la mikopo hiyo ya asilimia 10 haitakuwa lazima kikundi bali hata mtu mmoja ataweza kukopeshwa ili mradi ajulikane anakwenda kufanya nini.

Mhe Juliana Didas Masaburi mbunge viti maalumu CCM kupitia kundi la vijana