Storm FM

Mbunge awapongeza wananchi kwa kujitoa kutengeneza barabara

17 February 2026, 7:52 am

Mbunge jimbo la Geita mjini, mkoani Geita, Chacha Wambura akiwa pamoja na wananchi wakazi wa kata ya Bung’wangoko wakilima barabara. Picha na Ester Mabula

Mbunge jimbo la Geita mjini, mkoani Geita, Chacha Wambura amewapongeza wananchi kwa kujitoa kutengeneza miundombinu ya barabara huku akisema “katika kipindi cha uongozi wangu nitahakikisha barabara hii inatengenezwa kwa ubora zaidi ili kuondoa changamoto”

Na: Ester Mabula

Wananchi wa Kata ya Bung’wangoko wilayani Geita mkoani Geita wameungana na Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Mhandisi Chacha Wambura kukarabati kwa kulima barabara ilioyopo katika kata hiyo.

Hatua hiyo imekuja kufuatia miundombinu kuwa mibovu hali inayopelekea ajali za mara kwa mara na kuathiri shughuli za kijamii na kiuchumi kama wanavyobainisha

Sauti ya wananchi
Mbunge Chacha Wambura akiwa pamoja na wananchi wakazi wa kata ya Bung’wangoko wakilima barabara. Picha na Ester Mabula

Kufuatia jitihada hizo Mbunge Chacha ameahidi ndani ya kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake kuhakikisha anaboresha miundombinu ya barabara hiyo huku akiahidi tripu 50 za moramu pamoja na fedha taslimu kiasi cha shilingi laki 6 kwa ajili ya kuboresha zaidi eneo hilo.

Sauti ya mbunge Chacha Wambura
Mbunge wa jimbo la Geita mjini Chacha Wambura akizungumza na wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuhtimisha kazi. Picha na Ester Mabula

Katika hatua nyingine ameeleza dhamira yake ya kuanzisha mradi wa kulima nyanya ambao utawanufaisha vijana akieleza kuwa lengo lake ni kuhakikisha vijana wanafanya kazi ili kujikwamua kimaisha

Sauti ya mbunge Chacha Wambura
Mbunge Chacha Wambura akiwa na baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji na kata. Picha na Ester Mabula