Storm FM

Wapangaji wamlilia mwenye nyumba kufunga choo kwa zaidi ya siku 14

13 February 2026, 12:28 pm

Muonekano wa choo ambacho kimefungwa na mwenye nyumba kwa zaidi ya siku 14. Picha an Kale Chongela

“Kwenye mkataba wetu hauoneshi kama sisi wapangaji tunatakiwa kuchanga pesa ili kuweza kuzibua choo, hili jambo linapelekea mkanganyiko” – mmoja wa mpangaji

Na: Kale Chongela

Choo kinachotumiwa na wapangaji 10 katika nyumba inayomilikiwa na Bi. Jedida Kassim iliyopo mtaa wa Ujamaa kata ya Kalangalala  halamshauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita kimefungwa hali inayosabisha wapangaji hao kwenda kujisaidia kwa majirani.

Wapangaji hao wameiambia Storm FM kuwa choo hicho kimefungwa kwa muda wa zaidi ya siku 14 ambapo kwa mujibu wa maelezo yao wamesema mmiliki wa nyumba hiyo aliwataka wao kuchangia shilingi elfu 7 kila  mmoja ili gari la takaa liweze  kuvuta  maji taka katika choo hicho.

Sauti ya wapangaji

Mmiliki wa nyumba hiyo amekiri choo hicho kufungwa na kufafanua kuwa changamoto ni baadhi ya wapangaji kutumia choo hicho vibaya  ikiwemo kumwanga maji mara baada ya kufua nguo zao hali ambayo inachangia choo hicho kujaa mapema.

Sauti ya mwenye nyumba
Nyumba wanayoishi wapangaji waliolalamikia kufungwa choo na mwenye nyumba kwa zaidi ya siku 14. Picha na Kale Chongela

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw. Musa Mbaruku amekiri suala hilo kutokea katika mtaa wake na kueleza  kuwa baada ya kujiridhisha amemtaka mmiliki wa nyumba hiyo kufungua choo hicho ili wapangaji hao waweze kutumia.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa Ujamaa