Storm FM
Storm FM
9 February 2026, 10:55 am

“Uwepo wa bonanza hili si tu kwaajili ya kucheza michezo mbalimbali bali ni kuimarisha afya za mwili pamoja na mahusiano miongoni mwa wafanyakazi” – Dominic Marandu, mgeni rasmi.
Na: Ester Mabula
Wafanyakazi wa GGML pamoja na kampuni zilizopo ndani ya mgodi huo wameshiriki katika bonanza la michezo lililofanyika Februari 07, 2026 katika uwanja wa Nyankumbu girls uliopo halmashauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita.
Bonanza hilo limehusisha michezo mbalimbali ikiwemo kukimbiza kuku, kukimbia kwenye magunia, kukimbia na yai kwenye kijiko, mchezo wa kukaa kwenye viti, basketball,netball, volleyball pamoja na mpira wa miguu kwa wanaume ambapo timu ya GGM iliibiuka mshindi katika mpira wa miguu kwa kuifunga timu ya Infinity bao 1 kwa 0.

Mgemi rasmi katika tamasha hilo Bw. Dominic Marandu ambaye ni Kaimu mkurugenzi wa Rasilimali watu kutoka GGM, amesema lengo la bonanza hilo ni kuimarisha afya pamoja na mahusiano miongoni mwa wafanyakazi.
Viongozi wa GGM Sports Club Gueen Irene Fele ambae ni katibu msaidizi na Mwenyekiti Valence Ibrahim wameushukuru uongozi wa Mgodi pamoja na uongozi wa shule ya Nyankumbu girls kwa kuweza kufanikisha uwepo wa bonanza hilo kwani limesaidia kuwakutanisha wafanyakazi pamoja kwa lengo la kuimarisha mahusiano

