Storm FM
Storm FM
23 January 2026, 11:23 am

Shule ya msingi Ndalichako iliyopo katika kijiji na kata ya Bwanga, halmshauri ya wilaya ya Chato mkoani Geita ina jumla ya wa wanafunzi 1045
Na: Ester Mabula
Mbunge wa Jimbo la Chato Kusini Mhe. Paschal Lutandula ametoa bati 200 ili kuezeka jengo lenye vyumba vitatu katika shule ya msingi Ndalichako, iliyopo Kata ya Bwanga wilayani Chato mkoani Geita.
Akikabidhi bati hizo kwa niaba ya mbunge, Katibu wa Mbunge, Joseph James, amesema Mbunge Lutandula ataendela kugusa maeneo mbalimbali kama alivyoahidi ili kuweza kudumisha ushirikiano na wananchi ndani ya jimbo lake huku akisisitiza mabati hayo kutumika kwenye lengo lililokusudiwa.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Felister Shadrack ameeleza kufurahishwa na msaada huo akisema kuwa utasaidia kukamilisha zoezi la kuezeka majengo ya shule na kuchangia kupunguza tatizo la upungufu wa madarasa, hali itakayoongeza ufanisi wa ufundishaji na ujifunzaji.
Mwenyekiti wa kijiji cha Bwanga Fares Enelicko amesema msaada uliotolewa na mbunge utasaidia kuchochea ufanisi wa walimu kufundisha.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wazazi wenye wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo wameshukuru kwa msaada huo wakieleza namna ulivyowahamasisha kuchanga shilingi elfu 10 kila kaya kwaajili ya kusaidia gharama za matengenezo.
