Storm FM

Wakazi Nyantimba wamshukuru mbunge kukamilisha jengo la shule

5 January 2026, 12:58 pm

Muonekano wa Jengo la utawala linaloendelea kujengwa kwa ufadhili wa mbunge. Picha na Ester Mabula

“Kunipigia kura na kunichagua ni kunikopesha maendeleo ndani ya miaka mitano na nitahakikisha changamoto zilizo ndani ya uwezo wangu zinakwisha” – Mbunge Lutandula

Na: Ester Mabula

Wananchi wa kijiji cha Nyantimba kata ya  Nyarutembo halmashauri ya wilaya ya Chato mkoani Geita, wamemshukuru Mbunge wa Jimbo la Chato kusini Mhe. Paschal Lutandula kwa kuweza kukamilisha ujenzi wa jengo la utawala katika shule ya sekondari iliyopo katika kijiji cha Nyantimba.

Wanafunzi katika kijiji hicho wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya Kilometa 6 ili kupata elimu katika shule za maeneo jirani, ambapo wakizungumza kwa niaba ya wananchi wengineBi. Yuritha Panckras na Bw. Sylvanus Makeremo wametoa shukrani kwa mbunge huyo kwa kuweza kutatua changamoto hiyo.

Sauti ya wananchi
Yuritha Pankras, mkazi wa Nyantimba akizungumza na waandishi wa habaroi. Picha na Ester Mabula

Mkwasi Jonh ni Kaimu mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Chato amesema kuwa kwa muhula mpya wa masomo utakaoanza mwezi huu Januari jumla ya wanafunzi 75 wa kidato cha kwanza wataanza masomo katika shule hiyo.

Sauti ya kaimu mkurugenzi halmashauri ya Chato
Mbunge wa chato kusini Mhe. Paschal Lutandula akisisitiza jambo kwa wananchi (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Akizungumza baada ya kukabidhi mabati kwaajili ya ujenzi huo, ujenzi mbunge Lutandula amesema katika uongozi wake ataendelea kugusa wananchi wa jimbo hilo kwani wakati anaomba kura alikuatana na changamoto hiyo ya shule na kuahidi kuweza kuitatua ili kusaidia wanafunzi wa kijiji hicho kutotembea umbvali mrefu.

Sauti ya mbunge Paschal Lutandula
Muonekano wa baadhi ya majengo ya shule ya sekondari iliyopo kijiji cha Nyantimba. Picha na Ester Mabula