Storm FM

Wanawake zaidi ya 200 wakimbilia VETA Chato

18 July 2025, 7:20 pm

Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Geita akiwa na wanufaika wa mafunzo chuo cha VETA Chato. Picha na Kale Chongela.

Wanawake mkoani Geita wameendelea kuchangamkia fursa ya elimu ya ufundi katika vyuo mbalimbali vilivyopo mkoani humo ili kujikwamua kiuchumi.

Na Kale Chongela:

Zaidi ya wanawake 200 wakazi wa wilaya ya Chato mkoani Geita wanaonufaika na mafunzo ya ufundi stadi  katika chuo cha VETA  wilayani humo wameipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa ya mafunzo  hayo bila malipo.

Wanawake hao 240 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya ya Chato  wakizungumza na Storm FM chuoni hapo mbali nakuishukuru serikali kwa fursa hiyo wameahidi kutumia ujuzi huo kujikwamua kiuchumi nakusadia watu wengine.

Sauti ya wanufaika wa mafunzo Chato
Wanawake waliochangamkia fursa ya mafunzo chuo cha VETA wakiwa katika picha ya pamoja. Picha na Kale Chongela.

Mkuu wa chuo cha VETA  Chato Bi Liliani Mlimira amewapongeza wanawake hao kwa uthubutu huo huku akisema fani walizochangamkia ni pamoja na Uchakataji wa samaki,Upishi,Ufundi umeme na Ufundi bomba.

Sauti ya Mkuu wa VETA Chato

Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Mkoa wa Geita ambae ni Makamu mwenyekiti wa Wanawake na Samia Tanzania Bi Adelina Kabakama  amewasihi wananwake hao kutumia mafunzo hayo  kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya Mwenyekiti wanawake na Samia Geita
Muonekano wa mbele wa baadhi ya majengo ya chuo cha VETA Chato. Picha na Kale Chongela