Storm FM

Vikundi 100 vyapatiwa mkopo halmashauri ya manispaa ya Geita

15 May 2025, 5:12 pm

Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba akiwa na baadhi ya wanufaika wa mkopo. Picha na Ester Mabula

Jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 1.228 kimetolewa kwa vikundi 100 vinavyojumuisha makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kuweza kujikwamua kiuchumi kupitia miradi mbalimbali.

Na: Ester Mabula:

Hafla ya utoaji wa mikopo hiyo imefanyika leo Mei 15, 2025 katika ukumbi wa St. Aloysious mtaa wa Shilabela mjini Geita.

Awali, akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi, mkuu wa idara ya maendeleo ya Jamii manispaa ya Geita Robert Jackson Sungura ametaja idadi ya vikundi ambavyo vimepatiwa mkopo huo kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pamoja na kutaja mchanganuo wa kiasi kilichotolewa kwa kila kundi.

Sauti ya mkuu wa idara ya maendeleo manispaa ya Geita
Mkuu wa iadara ya maendeleo ya Jamii manispaa ya Geita, Robert Sungura. Picha na Ester Mabula

Mstahiki Meya wa halmashauri ya manispaa ya Geita Mhe. Costantine Morandi ameeleza kuwa kwa sasa halmashauri ya manispaa ya Geita imepiga hatua katika kiwango cha fedha kilichotolewa kutoka shilingi milioni 600 mwaka wa fedha uliopita hadi shilingi Bilioni 1.228 iliyotolewa leo.

Sauti ya mstahiki Meya Mhe. Costantine Morandi

Mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Abdallah Komba amesema fedha zilizotolewa zikalete tija kwa wanufaika ili kuweza kuzalisha makundi mengi zaidi ya watu watakaonufaika na mikopo hiyo, kwani dhamira ya serikali ni kufikia watu wengi zaidi.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba
DC Geita Mhe. Hashim Abdallah Komba akizungumza na wanufaika wa mkopo. Picha na Ester Mabula

Aidha Mhe. Komba ameelekeza shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira bora ya kuwanufaisha wananchi kupitia mikopo ya halmashauri inayotolewa kote nchini.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba

Baadhi ya wanaufaika wa mkopo huo wakizungumza kwa niaba wa wenzao Frank Bukela na Lucia Khalfan wametoa shukrani kwa Rais Samia kwa kupatiwa mikopo hiyo.

Sauti ya wanufaika wa mkopo
Baadhi ya wanufaika wa mkopo uliotolewa leo kwa vikundi 100 manispaa ya Geita. Picha na Ester Mabula