Storm FM

RC Geita akabidhi bima za afya 102 kwa watoto yatima

11 April 2025, 11:32 am

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela akizungumza baada ya kukabidhi bima za afya.

Watoto 102 wa kituo cha kulea watoto yatima cha moyo wa huruma kilicho chini ya kanisa katoliki geita wamekabidhiwa bima za afya za NHIF jana April 09 2025.

Na: Daniel Magwina:

Akizungumza katika zoezi hilo la kukabidhi bima hizo mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela amesema bima hizo zitakwenda kuwasaidia watoto hao kwaajili ya matibabu huku akiwaomba wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kusaidia watoto wasiojiweza.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela

Naye meneja wa NHIF mkoa wa Geita Elias Odhiambo amesema bima hizo ni za mwaka mmoja na kwamba watoto hao watapata huduma kuanzia ngazi ya awali mpaka huduma za kibingwa

Sauti ya meneja wa NHIF Elias Odhiambo
RC Geita (kati), Meneja wa NHIF mkoa wa Geita (kushoto) na Sister Maria Lauda (kulia) Picha na Magwina

Kwa upande wake mkurugenzi wa kituo hicho cha moyo wa huruma Sister Maria Lauda amesema bima hizo zitawasaidia kupunguza gharama za matibabu kwa watoto hao.

Sauti ya mkurugenzi Sister Maria Lauda

Bima za afya kwa watoto yatima ni ngao muhimu inayowahakikishia huduma bora za afya bila mzigo wa gharama kubwa.

Pia Bima inawezesha kupata matibabu kwa wakati, kuzuia magonjwa sugu, na kuboresha afya yao kwa ujumla.Pia bima inasaidia kupunguza changamoto kwa walezi wa vituo vyao, kuwapa nafasi ya kuzingatia malezi na elimu.

Baadhi ya watoto yatima wanaopatiwa malezi kituo cha Moyo wa huruma. Picha na Daniel Magwina