Storm FM

Wananchi wajitolea kuziba maeneo korofi ya barabara

5 April 2026, 20:03

Wananchi wakibeba mawe kwaajili ya kuziba maeneo korofi ya barabara. Picha na Kale Chongela

“Hii barabara imekuwa ikitupa usumbufu mkubwa sana kwahiyo imetulazimu kuweka mawe ili kuondoa usumbufu wakati wa kutumia” – Mwananchi

Na: Kale Chongela

Wananchi wa mtaa wa Nyantorotoro B, kata ya Nyankumbu, halmashauri ya Manispaa ya Geita, wameonesha mshikamano kwa kujitolea kushiriki katika uboreshaji wa sehemu korofi za barabara inayounganisha mtaa wa Nyantorotoro ubaoni hadi mtaa wa Mbabani.

Baadhi ya wananchi wakizungumza na Storm FM wamesema hatua hiyo imekuja kufuatia changamoto ya muda mrefu ya miundombinu mibovu, hasa kwa baadhi ya maeneo yalikuwa yakipitisha maji na kusababisha uharibifu wa barabara  kwa  watumiaji wa vyombo vya moto.

Sauti ya wananchi

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw. Juma  Ally amepongeza juhudi hizo za wananchi huku akibainisha kuwa ushirikiano huo ni mfano mzuri wa uzalendo na kujitolea katika kuleta maendeleo ya jamii.

Sauti ya mwenyekiti
Shughuli ya kuweka mawe kwenye eneo korofi la barabara ikiendelea. Picha na Kale Chongela

Kaimu meneja wa wakala wa barabara za mjini na vijijini TARURA Wilaya ya Geita Mhandisi Gadi Loi  akizungumza kwa njia ya simu amekiri kuwepo wa changamoto  hiyo na kueleza kuwa eneo hilo tayari wameliombea fedha kiasi cha shilingi  milioni 170 kwaajili ya kuweka molamu.

Sauti ya kaimu meneja wa TARURA