Storm FM

Motisha wasichana kupenda masomo ya sayansi yaongezeka

05/03/2026, 18:30

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bugurula wakiendelea kupewa mafunzo. Picha na Ester Mabula

GGML Mentorship program ilianzishwa mwaka 2020 ikiwa na lengo la kumsaidia msichana kutimiza ndoto zake kitaaluma sambamba na kumjengea uwezo wa kujiamini.

Na: Ester Mabula

Jumla ya shule sita za sekondari ambazo ni Nyalwanzaja, Kamena, Kasota, Bugando, Bugurula na Butundwe zimefikiwa na mpango wa GGML Mentorship program ambao unalenga kutoa elimu ya utambuzi kwa wasichana ili waweze kutimiza ndoto zao.

Mpango huo wa kutoa elimu mafunzo na kuwajengea wasichana uwezo wa kujiamini ulianzishwa mwaka 2020 ambao umetajwa kuwa chachu ya kuongeza ufaulu kwa wasichana kama wanavyobainisha Lilian Hamis mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya Bugurula na Doris Alfred mwanafunzi wa kidato cha tano shule ya sekondari Butundwe.

Sauti ya wanafunzi
Mkuu wa shule ya sekondari Butundwe Mwl. Happiness Manyama akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Wakuu wa shule za sekondari Butundwe na Bugurula Mwl. Happines Manyama na Embola Palangyo wanaeleza kuwa mpango huo umekuwa na tija kitaaluma kwa watoto wa kike sambamba na kuchochea ari ya kupenda masomo ya sayansi.

Sauti ya wakuu wa shule

Akielezea dhamira ya kuanzisha mpango huo Msimamizi wa Rasilimali watu kutoka GGML Khadija Kisatu amesema, mpango huo unasimamiwa na wafanyakazi wanawake wa GGM ambapo ulianzishwa baada ya kubaini kuwa wasichana wanakabiliwa na vikwazo mbalimbali vinavyopelekea kukwamisha ndoto zao.

Sauti ya msimamizi wa Rasilimali watu kutoka GGML
Khadija Kisatu, msimamizi wa Rasilimali watu kutoka GGML akieleza dhamira ya mpango huo. Picha na Ester Mabula