Storm FM
Storm FM
26/02/2026, 15:47

Licha ya mvua kuleta neema kwa wakulima , hali imekuwa tofauti kwa wakazi wa Nyatorotoro B, kata ya Nyankumbu wilayani na mkoani Geita kwani wanalazimika kulala wakiwa wamesimama.
Na: Ester Mabula
Kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini, Wakazi wa mtaa wa Nyantorotoro B kata ya Nyankumbu wilayani na mkoani Geita wameiomba serikali kuwasaidia kutafuta suluhu ya kudumu juu ya uhaba wa miundombinu ya barabara hali inayopelekea changamoto ya maji kujaa katika makazi yao pindi mvua zinaponyesha.
Wakizungumza na Storm FM, baadhi ya wakazi wa eneo hilo wameeleza kuwa mvua zinaponyesha hali hiyo imekuwa ikihatarisha usalama wao pamoja na uharibifu wa mali na makazi yao.

Diwani wa kata ya Nyankumbu Paschal Kimisha Sukambi amewaomba wataalam mbalimbali kutoka manispaa ya Geita kufika eneo hilo ili waweze kutafuta suluhu ya tatizo hilo.

Licha ya malalamiko ya wananchi, kwa mujibu wa maelezo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Geita imeonekana eneo lile ni mkondo wa maji na hivyo ametoa rai kwa wananchi kuzingatia umbali wa mita 60 pindi wanapojenga nyumba za makazi,
