Storm FM

Manispaa ya Geita yapitisha bajeti ya Tsh. bil. 78.8 kwa mwaka 2026/2027

27 January 2026, 5:10 pm

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Geita Yefred Myenzi akizungumza katika kikao cha baraza. Picha na Ester Mabula

Baraza la madiwani la halmashauri ya Manispaa ya Geita leo Januari 27, 2026 limejadili na kupitisha rasimu ya bajeti kisasi cha shilingi bilioni 78,811,212,825.7 kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Na: Ester Mabula

Bajeti hiyo ina ongezeko la 8.3% zaidi ya ile ya mwaka wa fedha 2025/2026 ambapo matarajio katika bajeti ya mwaka huu ni kugharamia na kuboresha miradi mbalimbali ya maendeleo kupitia vipaumbele vilivyotajwa ikiwemo afya, miundombinu ya barabara pamoja na elimu.

Akizungumza wakati wa kikao hicho Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya insmanispaa ya Geita Yefred Myenzi ametaja mchanganuo wa bajeti hiyo kwa kuainisha kiwango cha matumizi kwa kila eneo.

Sauti ya mkurugenzi mtendaji manispaa ya Geita
Mstahiki Meya manispaa ya Geita Leonard Bugomola akizungumza wakati wa kikao. Picha na Ester Mabula

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Geita Leonard Bugomola amewataka madiwani na watendaji kuendelea kuchapa kazi kwa bidii huku akisema ukuaji wa manispaa uendane sambamba na uvumbuzi wa vyanzo vipya vya mapato kupitia miradi mbalimbali.

Sauti ya mstahiki meya manispaa ya Geita

Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita Bi. Lucy Beda ameipongeza halmashauri ya Manispaa ya Geita kwa juhudi zake za kuendelea kupeleka fedha kwenye miradi ya maendeleo akisema hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma kwa wananchi na kuleta tija katika matumizi ya rasilimali za UMMA.

Sauti ya katibu tawala wilaya ya Geita

Akizungumza kwa niaba ya madiwani, Reuben Sagayika ambaye ni diwani wa kata ya Kalangalala amepongeza bajeti hiyo akieleza kuwa imelenga maeneo muhimu kwa wananchi.

Sauti ya diwani kata ya Kalangalala
Baadhi ya madiwani wakiwa katika kikao cha kupitisha rasimu ya bajeti leo. Picha na Ester Mabula