Storm FM
Storm FM
26 January 2026, 1:15 pm

“Tunashukuru malezi na mafundisho aliyotupa baba yetu na tutayaendeleza kwa uzao wake ikiwa ni kuendelea kuheshimu watu wote katika Jamii” – Mtoto wa marehemu
Na: Kale Chongela
Historia ya kuishi duniani ya Mzee Jacob Chigabilo Katukula mkazi wa mtaa wa Nyamakale kata ya Nyankumbu, halmshauri ya manispaa ya Geita mwenye umri wa miaka115 imefikia tamati Januari 19, 2026 baada ya kufariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Geita.
Wakazi wa Geita wameungana na familia katika ibada maalum ya kumuaga mpendwa wao Mzee Chigabilo ibada ambayo imefanyika nyumbani kwa marehemu ambapo ibada hiyo imeongozwa na Padri Silas Haki kutoka parokia ya Mtakatifu Antony wa Padua Nyarubele.
Mzee Chigabilo ameacha watoto 34, wajukuu 206, vitukuu 624, vilembwe 1009, vilembwekeze 116.
Taarifa ya Kale Chongela inaeleza zaidi.

