Storm FM

TISEZA yafanya ziara mkoani Geita kuhamasisha uwekezaji

20 January 2026, 12:50 pm

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TISEZA, Dkt. Aziz Ponary Mlima akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Jumla ya miradi 901 yenye thamani ya Tsh. bilioni 9.31 kwa mwaka 2024, na miradi 927 kwa mwaka 2025 yenye thamani ya Tsh. bilioni 11 ambapo jumla ya miradi 469 inamilikiwa na watanzania sawa na asilimia 51%.

Na: Ester Mabula

Watanzania wametakiwa kuendelea kutumia fursa za uwekezaji zilizizopo nchini sambamba na kusajili miradi yao  kwenye mamlaka ya uwekezaji na maeneo maalumu ya  kiuchumi (TISEZA) hatua itakayowawezesha kukua, kupata tija ya kiuchumi na kupata nafuu ya msamaha wa kodi kwa bidhaa ambazo zinatumika kwenye miradi iliyosajiliwa.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa TISEZA, Dkt. Aziz Ponary Mlima jana Januari 19, 2026 akiwa katika ziara mkoani Geita ya kampeni ya kitaifa ya uhamasishaji uwekezaji wa ndani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji kwa vitendo Mpango wa Taifa wa Maendeleo kwa miaka mitano (FYDP) inayolenga kutekeleza azma ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kufungua nchi kwa kuhamasisha uwekezaji.

Sauti ya mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TISEZA

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela akizungumza mapema na uongozi wa TISEZA amepongeza uwepo wa ziara hiyo inayolenga kupita mikoa mbalimbali nchini ili kujenga uelewa akieleza hatua hiyo itasaidia kuamsha ari ya wananchi kujisajili.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela
RC Geita (kulia) akikabidhiwa zawadi na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TISEZA mara baada ya kufika ofisini kwa mkuu wa mkoa. Picha na Ester Mabula

Mwekezaji katika sekta ya uchimbaji wa dhahabu mkoani Geita ambaye pia ni mmiliki wa hoteli, Leonard Bugomola amewasihi watanzania kusajili miradi yao akieleza manufaa anayopata  huku mwekezaji wa uchenjuaji wa dhahabu Bi. Zahida Abdalah akiipongeza serikali kwa kuendelea kurahisisha michakato ya upataji vifaa mbalimbali kwaajili ya shughuli zao

Sauti ya wawekezeji
Leonard Bugomola, mwekezaji katika sekta ya madini na mmiliki wa hoteli Geita. Picha na Ester Mabula

Pamoja na ziara hiyo ya kukagua miradi ya wawekezaji,  mamlaka ya uwekezaji na maeneo maalumu ya  kiuchumi (TISEZA)  pia itaendesha semina na makongamano ya Uwekezaji kwa makundi mbalimbali katika jamii yanayojumuisha wajasiriamali wadogo na wa Kati (SMEs), wafanyabiashara, vijana, wanahabari, maafisa wanaosimamia viwanda, biashara na uwekezaji katika sekretarieti za mikoa na halmashauri.

Bi. Zahda Abdallah, mwekezaji katika shughuli ya uchenjuaji wa dhahabu mkoani Geita. Picha na Ester Mabula