Storm FM

Diwani wa Nyanguku atangaza kiama kwa wazazi wakaidi

15 January 2026, 4:19 pm

Diwani wa kata ya Nyanguku Elias Ngole akizungumza na wazazai (hawapo pichani) waliofika shuleni. Picha na Ester Mabula

Leo ni siku ya pili tangu kuanza kwa muhula mpya wa masomo ambapo shule zimefunguliwa Januari 13, 2026 kote nchini.

Na: Ester Mabula

Diwani wa Kata ya Nyanguku ambaye pia ni Naibu Meya wa halmashauri ya manispaa ya Geita amewaasa wazazi na walezi kujiepusha na vitendo vya kuwakatisha masomo watoto wao na badala yake wawapeleke shule ili wapate elimu.

Mhe. Ngole ametoa kauli hiyo leo Januari 15, 2026 akiwa katika shule ya sekondari Nyanguku iliyopo halmashauri ya manispaa ya Geita, ambapo amekuwa na utaratibu wa kukabidhi madaftari kwa wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza wanaojiunga katika shule hiyo.

Madaftari yaliyokabidhiwa kwa wanafunzi 90 wa kidato cha kwanza walioripoti shuleni. Picha na Ester Mabula

Amewasisitiza wazazi kuacha tabia ya kuwaozesha mabinti sambamba na kuhusisha watoto na shughuli za kilimo, akisema  mustakabali wa maendeleo duniani kote unategemea elimu.

Sauti ya Diwani wa Nyanguku Elias Ngole

Baadhi ya wazazi waliopeleka watoto wao katika shule hiyo Onesmo Mashishanga na Getruda Stephano wamemshukuru Diwani huyo kwa kuendelea kuwasadia wazazi kununua madaftari wakisema hatua hiyo inaleta motisha zaidi.

Sauti ya wazazi
Wazazi la walezi wa wanafunzi waliojitokeza shuleni kwenye zoezi la kugawa madaftari. Picha na Ester Mabula

Afisa elimu kata ya Nyanguku Innocent Yasese amesema Jumla ya wanafunzi 90 wa kidato cha kwanza wameripoti shuleni hapo kuanza kidato cha kwanza ambapo amesema hatua hiyo ya kutoa madaftari   inayofanywa na diwani inaongeza motisha ya wanafunzi kusoma.

Sauti ya Afisa elimu kata ya Nyanguku
Muonekano wa juu wa Jengo la utawala lililopo katika shule ya sekondari Nyanguku. Picha na Ester Mabula