Storm FM

Kijana ashambuliwa kwa kipigo akihisiwa ni mwizi

14 January 2026, 10:41 am

Askari polisi wakisaidiana na wananchi kumbeba kijana aliyeshambuliwa kwa kipigo. Picha na Ester Mabula

“Jamani mtu kama unaona kakosea ni bora kumpeleka kwenye mamlaka husika na sio kumpiga na kumtelekeza kama hivi” – Mwananchi

Na: Ester Mabula

Kijana mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 ambaye ameshindwa kuzungumza vizuri huku akishindwa kutaja jina lake amedai kupigwa na watu usiku akihisiwa kuwa ni mwizi.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Januari 13, 2026 ambapo kijana huyo amekutwa akiwa amelala katika uwanja  wa mpira wa shule ya sekondari Nyanza, mtaa wa Nyanza, halmashauri ya manispaa ya Geita ambapo ameshindwa kuzungumza akidai kuishiwa nguvu.

Kijana akiwa amelala huku akishindwa kusimama baada ya kushambuliwa kwa kipigo. Picha na Ester Mabula

Wakizungumza baadhi ya wananchi ambao walijitokeza kushuhudia tukio hilo Lucas John na Elizabeth Mihayo wameeleza namna walivyomuona mtu huyo

Sauti ya wananchi
Sehemu ya miguu ambayo imedaiwa kujeruhiwa na kupelekea kushindwa kutembea. Picha na Ester Mabula

Hamis abdallah ni Mjumbe wa serikali ya mtaa wa Nyanza ameeleza hatua walizochukua juu ya tukio hilo ambapo amesema walihusisha Jeshi la polisi kwa hatua zaidi.

Sauti ya mjumbe wa serikali ya mtaa

Viongozi wa serikali ya mtaa akiwemo Mwenyekiti walifanya jitihada za kulifikia Jeshi la poisi kwa hatua zaidi ambapo hata hivyo Jeshi la polisi limefika eneo la tukio na kumchukua kijana huyo kwa msaada zaidi.

Gari la Jeshi la Polisi lililofika eneo la tukio kwaajili ya kumchukua kijana huyo. Picha na Ester Mabula