Storm FM

Sagayika kutoa madaftari kwa watoto wenye uhitaji

10 January 2026, 6:38 pm

Diwani wa kata ya Kalangalala Reube Sagayika akizungumza na wana habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Januari 13, 2026 shule zote nchini zitafunguliwa na kuanza rasmi kwa mhula mpya wa masomo baada ya kukamilika sikukuu za mwisho wa mwaka.

Na: Ester Mabula

Diwani wa kata ya Kalangalala wilayani na mkoani Geita Reuben Sagayika leo Januari 10, 2026 amefanya ziara ya kutembelea shule ya msingi Kalangalala ili kufuatilia zoezi la uandikishaji wanafunzi shuleni hapo kwa ajili ya mhula mpya wa masomo unaotarajiwa kuanza Januari 13, 2026.

Akiwa shuleni hapo Sagayika ameeleza kuwa kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto atakuwa na zoezi la kugawa vifaa vya shule kwa wanafunzi wenye uhitaji siku ya Jumatatu Januari 12, 2025 ambapo zoezi hilo litafanyika katika ofisi ya kata hiyo.

Sauti ya diwani wa kata ya Kalangalala
Diwani kata ya Kalangalala Reuben Sagayika akipewa maelekezo na Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kalangalala wakati wa ziara. Picha na Ester Mabula

Aidha ameeleza kuwa ziara za kutembelea shule zilizopo katika kata hiyo ni zoezi endelevu ambalo litasaidia kuweza kubaini changamoto zilizopo kwenye shule hizo kwaajili ya utatuzi.

Sauti ya diwani wa kata ya Kalangalala
Kaimu afisa elimu kata ya Kalangalala Bi. Regina Ketau akizungumza na wana habari. Picha na Ester Mabula

Kaimu Afisa Elimu kata ya Kalangalala  Regina Comas Ketau ameeleza kuwa kata hiyo ina jumla ya shule 9 za msingi ambapo hadi sasa jumla ya wanafunzi 1640 wameandikishwa huku kukiwa na matarajio makubwa ya kuandikisha kwa asilimia 100.

Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kalangalala Mwl. Sospter Luzige akizungumza na wana habari. Picha na Ester Mabula

Kaimu mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kalangalala Mwl. Sospter Luzige amewasisistiza wazazi kupeleka watoto kuandikisha na kuacha kuwapeleka katika shule za mitaani huku Katibu wa Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi kata ya kalangalala Richard Nzagamba wa akitoa pongezi kwa Diwani huyo kwa kuw]akumbuka wanafunzi wenye uhitaji.

Sauti ya Kaimu mkuu wa shule na Mwenezi wa kata
Katibu wa Mwenezi wa CCM kata ya Kalangalala Richard Nzagamba akizungumza na wana habari. Picha na Ester Mabula