Storm FM

Mpango wa chakula kila shule Nyang’hwale umetiki

9 January 2026, 4:37 pm

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale akiwa katika ukaguzi wa mashamba ya shule. Picha na Mrisho Sadick

Zaidi ya wanafunzi 5,700 kutoka shule saba za msingi na shule moja ya sekondari ndio wanufaika wa moja kwa moja wa mpango huo.

Na Mrisho Sadick:

Kata ya Shabaka wilayani Nyang’hwale mkoani Geita imelima jumla ya ekari 41 za mahindi na viazi lishe ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale wa kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa chakula mashuleni kwa mwaka mzima.

Akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa mpango huo katika Kata zote Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Grace Kingalame akiwa katika Kata ya Shabaka amesema zoezi hilo linafanyika katika shule zote 74 za msingi na sekondari zilizopo wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale akizungumza na Storm FM baada ya ziara yake ya kukagua mashamba ya shule. Picha na Mrisho Sadick

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Kata ya Shabaka amesema zaidi ya wanafunzi 5,700 kutoka shule saba za msingi na shule moja ya sekondari ndio wanufaika wa moja kwa moja wa mpango huo huku Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amesema mpango huo umeanza kuonesha matokeo chanya tangu ulipoanza kutekelezwa.

Shamba la mahindi katika shule ya msingi Ihushi Kata ya Shabaka. Picha na Mrisho Sadick

Mkuu wa wilaya kwa kushirikiana na mkurugenzi wa halmashauri wamenunua mbegu kilo  zaidi ya1,400 kupitia mapato ya ndani nakuzigawa kwenye shule zote kwa wastani wa kilo 16 kila shule kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo ambao umefanikiwa kwa asilimia kubwa.

Sauti ya Ripoti kamili ya stori hii na Mrisho Sadick