Storm FM

Wananchi wamshukuru Diwani utatuzi kero ya mashimo stendi ya Geita

8 January 2026, 7:01 pm

Diwani wa kata ya Kalangalala Reuben Sagayika akiangalia marekebisho yanayoendelea. Picha na Ester Mabula

“Lengo ni kuhakikisha abiria na watumiaji wa barabara wanakuwa katika hali ya usalama pindi wanapotumia stendi hii hususani kipindi cha mvua” – Reuben Sagayika

Na: Ester Mabula

Wananchi na watumiaji wa kituo kikuu cha mabasi mkoa wa Geita wameishukuru serikali kwa kushirikiana na Diwani wa kata ya Kalangalala kwa kuchukua hatua ya kufukia mashimo yaliyokuwa yakisababisha usumbufu mkubwa kwa muda mrefu.

Mashimo hayo yalitokana na uharibifu wa miundombinu kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha, hali inayosababisha usumbufu wakati wa utumiaji wa kituo hicho cha mabasi.

Mwenyekiti wa stendi ya mabasi Geita Godfrey Joseph akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Wakizungumza na Storm FM wameipongeza serikali na kumshikuru diwani kwa kuchukua hatua kwa haraka ya kutatua kero hiyo kama anavyobainisha mwenyekiti wa stedni hiyo Godfrey Joseph.

Sauti ya mwenyekiti wa stendi

Mmoja wa madereva pamoja na abiria ameeleza hatua hiyo iliyochukuliwa itasaidia kupunguza usumbufu kwa madereva pamoja na abiria.

Sauti ya dereva na abiria
Diwani wa kata ya Kalangalala Reuben Sagayika akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Diwani wa Kata ya Kalangalala, Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Mhe. Reuben Sagayika mapema leo Januari 08, 2025 ametembelea stendi hiyo na kujionea hatua za marekebisho zinazoendelea akisema lengo ni kuhakikisha stendi inakuwa salama na rafiki kwa watumiaji wote, hasa katika kipindi cha mvua.

Sauti ya Diwani wa Kalangalala