Storm FM

Mbunge Chato Kusini awakumbuka wagonjwa sikukuu ya krismasi

26 December 2025, 2:07 am

Baadhi ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika kituo cha Afya Bwanga. Picha na Ester Mabula

“Ofisi ya mbunge jimbo la Chato Kusini itaendelea kushirikiana na wananchi katika mambo mbalimbali kwaajili ya maendeleo ya jimbo letu” – Joseph James, Katibu wa Mbunge

Na: Ester Mabula

Mbunge wa Jimbo la Chato kusini Paschal Lutandula amewakumbuka wagonjwa wanaopatiwa huduma katika kituo cha Afya Bwanga kwa kuwaandalia chakula cha pamoja na kuwakabidhi mahitaji mbalimbali.

Mahitaji hayo yamekabidhiwa Disemba 25, katika maadhimisho ya sikukuu ya Christmass, katika kituo cha Afya Bwanga ambapo makabidhiano yameongozwa na Diwani wa Kata ya Bwanga Bw. Sanane Chai ambaye ametoa wito kwa viongozi wengine kuendelea kuikumbuka Jamii kwa mahitaji mbalimbali.

Sauti ya diwani wa kata ya Bwanga Bw. Sanane Chai
Mganga mfawidhi kituo cha afya Bwanga, Dkt. Enos Kasongi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Akizungumza Dkt. Enos Kasongi, ambaye ni Mganga mfawidhi wa  kituo cha Afya Bwanga ameeleza jumla ya watoto 16 wamezaliwa sikukuu ya christmass katika kituo hicho na kutoa pongezi kwa mbunge kwa kuweza kuikumbuka Jamii.

Sauti ya mganga mfawidhi Dkt. Enos Kasongi

Baadhi ya wagonjwa ambao ni akina mama waliojifungua watoto akiwemo Fatuma Hamis na Ester Bukeye wamepongeza hatua hiyo na kumshukuru kwa kuweza kuwakumbuka katika siku hiyo muhimu ya Christmas.

Sauti ya baadhi ya wagonjwa
Diwani wa kata ya Bwanga Sanane Chai akikabidhi zawadi kwa mzazi, kulia ni katibu wa Mbunge Joseph James. Picha na Ester Mabula

Katibu wa Mbunge Joseph James amesema hatua hiyo imelenga kurejesha tabasamu kwa wananchi wa Chato kusini na kwamba ofisi ya Mbunge itaendelea kushirikiana na wananchi katika Nyanja mbalimbali.

Sauti ya katibu wa mbunge Joseph James
Katibu wa mbunge jimbo la Chato kusini Bw. Joseph James akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) . Picha na Ester Mabula