Storm FM

Maafisa maendeleo Geita wapewa maagizo mazito

18 November 2025, 12:21 pm

Maafisa maendeleo kutoka mkoa wa Geita wakiwa kwenye kongamano lao. Picha na Mrisho Sadick

Fursa ya ufugaji wa Samaki kwa kutumia vizimba iliyokuwa haitazamwi sana kwasasa imekuwa kimbilio

Na Mrisho Sadick:

Serikali Mkoani Geita imewataka maafisa maendeleo kuhakikisha wanakuwa daraja muhimu la kuwakwamua Wananchi kiuchumi kwa kuibua fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye maeneo yao ikiwemo ufugaji wa Samaki kupitia vizimba.

Katibu tawala wa Mkoa wa Geita Mohamed Gombati ametoa maagizo hayo kwenye Kongamano la kwanza la maafisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Geita lililofanyika Manispaa ya Geita huku afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Geita Martha Kaloso akisema kongamano hilo litakwenda kuongeza uwajibikaji kwa jamii kwa maafisa maendeleo hao.

Katibu tawala wa Mkoa wa Geita Mohamed Gombati akizungumza kwenye kongamano la maafisa maendeleo. Picha na Mrisho Sadick

Kwa upande wake Carlos Gwamagobe Kutoka Wizara ya maendeleo ya Jamii amewataka maafisa maendeleo hao kuendelea kuwasaidia wananchi kuchangamkia fursa zingine za uchumi siyo kutegemea shughuli za uchimbaji wa madini pekee.

afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Geita Martha Kaloso akiwa kwenye kongamano la maafisa maendeleo mkoa. Picha na Mrisho Sadick

Maafisa maendeleo wanaotoka Kata zinazopakana na ziwa Victoria wamesema fursa ya ufugaji wa Samaki kwa kutumia vizimba iliyokuwa haitazamwi sana kwasasa imekuwa kimbilio Kutokana na Elimu ambayo wanaendelea kuitoa.

Kaulimbiu ya Kongamano hilo ni – Uchechemuzi ni dira ya matokeo chanya kwa Jamii.

Ripoti kamili na Mrisho Sadick