Storm FM

AAFP yasema daktari akizuia maiti anawekwa kwenye jeneza yeye

15 October 2025, 3:07 pm

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Wakulima Tanzania (AAFP) akiwa Katoro Geita. Picha na Mrisho Sadick

Ngombalemwiru ameeleza kuwa serikali atakayoiunda itaweka mfumo rafiki wa huduma za afya utakaolenga utu na heshima ya binadamu.

Na Mrisho Sadick:

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Wakulima Tanzania (AAFP) Kunje Ngombalemwiru ameahidi kuondoa kabisa ada zinazotozwa hospitalini kwa familia zinazochukua miili ya wapendwa wao waliopoteza maisha.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Karoro wilayani Geita Oktoba 14,2025 Ngombalemwiru amesema utaratibu huo umekuwa chanzo cha mateso kwa wananchi wengi hasa wa kipato cha chini wanaokabiliwa na gharama kubwa wakati wa majonzi.

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Wakulima Tanzania (AAFP) akiwa Katoro Geita. Picha na Mrisho Sadick

Ngombalemwiru ameeleza kuwa serikali atakayoiunda itaweka mfumo rafiki wa huduma za afya utakaolenga utu na heshima ya binadamu akisisitiza kuwa hospitali hazipaswi kuwa chanzo cha mzigo kwa wananchi bali pa kutoa faraja na huduma bora.

Sauti ya Mgombea Urais AAFP

Katika hatua nyingine mgombea Urais huyo amesema endapo atachaguliwa kuwa Rais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, atatoa trekta kwa kila kaya 10 za wakulima ikiwa ni mkakati wa kukifanya kilimo kuwa chanzo kikuu cha uchumi wa taifa.

Sauti ya Mgombea Urais AAFP
Wakazi wa mji wa Katoro waliojitokeza kwenye kampeni za chama cha AAFP Katoro Geita. Picha na Mrisho Sadick