Storm FM

UDP yaahidi kusimamia rasilimali za nchi

16 September 2025, 11:10 am

Mgombea urais kupitia tiketi ya UDP Saumu Rashid akizungumza na wananchi (hawapo pichani). Picha na Edga Rwenduru

Vyama mbalimbali vya siasa nchini vimeendelea na kampeni ikiwa ni njia ya kunadi sera na mipango yao kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Na: Edga Rwenduru

Chama cha United Democratic Party (UDP) kimewaahidi watanzania kusimamia rasilimali za nchi  kwa uzalendo ili kila mwananchi afaidike na uwepo wa rasilimali hizo.

Akiwa mkoani Geita, mgombea wa kiti cha urais kupitia chama hicho Saumu Rashid ameahidi kuwa iwapo chama chake kitapewa dhamana ya kuongoza nchi, serikali yake itaweka mkazo katika kuinua uchumi wa Watanzania pamoja na kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha zaidi wananchi.

Sauti ya mgombea urais UDP
Baadhi ya wafuasi na wanachama wa UDP walivyompokea mgombea Urais. Picha na Edga Rwenduru

Kwa upande wake, mgombea mwenza wa urais kupitia chama cha UDP, Juma Hamis Faki, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura kwani  ni zoezi la kidemokrasia.

Sauti ya mgiombea mweza Urais UDP

Baadhi ya wananchi wa mkoa wa Geita aliojitokeza kusikiliza sera za chama cha UDP wameeleza kuridhishwa na sera za mgombea huyo.

Sauti ya baadhi ya wananchi
Baadhi ya wafuasi wa chama cha UDP wakiwa na mabango ya wagombea wa chama hicho. Picha na Edga Rwenduru