Storm FM

Wanafunzi Geita watembelea wanyamapori Chato

15 September 2025, 12:39 pm

Wanafunzi na walimu wakipewa maelekezo baada ya kufika shamba la wanyamapori. Picha na Kale Chongela

“Tunawashuru walimu kwa kutuandalia safari hii kwani imekuwa yenye tija kwetu katika kufahamu tabia za wanyama” – Mwanafunzi

Na: Kale Chongela

Wanafunzi wa shule ya msingi Mkoani iliyopo kata ya Kalangalala, halmashauri ya manispaa ya Geita wametembelea shamba la wanyama pori lililopo wilaya ya Chato mkoani Geita lenye ukubwa wa ekari 2500.

Wakizungumza na Storm FM baadhi ya wanafunzi ambao wametembelea shamba hilo la wanayama pori wamesema fursa hiyo imewajengea uelewa juu ya mambo mbalimbali kuhusu wanyama ikiwemo kufahamu namna ambavyo maisha ya wanyama yalivyo.

Sauti ya wanafunzi wa shule ya msingi Mkoani

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mkoani Mwl. Hubert Revelian amesema lengo la  kuwapelekea wanafunzi katika shamba hilo la wanyama pori ni  kuwasaidia kujifunza kwa vitendo juu ya wanyama pori.

Sauti ya mwalimu mkuu Hubert Revelian
Wanyama aina ya twiga wakiwa katika shamba la wanyama pori Chato. Picha na Kale Chongela

Mhifadhi wa wanyama pori katika shamba hilo Bw. Seithi Elias Mashini amesema katika shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 2500 wapo wanyama mbalimbali ikiwemo twiga, pundamilia, swala na ngiri huku akiwasihi wananchi kutembelea shamba hilo la wanyama pori.

Sauti ya mhifadhi wa wanyamapori
Wanyama aina ya pundamilia wakiwa katika shamba la wanyamapori Chato. Picha na Kale Chongela