Storm FM

Mwenge waridhishwa na mradi wa visima Nyangh’wale

4 September 2025, 10:38 am

Shughuli ya ukaguzi wa mradi wa visima vitano vya maji Nyangh’wale ikiendelea. Picha na Kale Chongela

Mwenge wa uhuru ukiwa wilaya ya Nyangh’wale  umetembelea, kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye jumla ya miradi 11 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.

Na: Kale Chongela

Mwenge wa uhuru umeridhishwa na ujenzi wa mradi wa visima vitano vya maji katika kata ya Shabaka, halmashauri ya wilaya ya Nyangh’wale vinavyotarajiwa kuondoa changamoto ya maji kwa wakazi wa eneo hilo.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ndugu Ismail Ally Ussi  baada ya kukagua mradi huo ameridhishwa na utekelezaji wa mradi na kwamba  ipo haja ya wananchi kuendelea kushirikiana na viongozi katika kulinda miundombinu ya maji ili iweze kuduma kwa muda mrefu.

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale  Mhe. Grace kingalame ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha katika wilaya hiyo ili kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

DC Nyangh’wale Grace Kingalame akimtwika ndoo ya maji mkazi wa Shabaka. Picha na Kale Chongela

Kwa upande wake Kaimu meneja wa RUWASA  Mhandisi Suzana Gogadi amesema vijiji vitano vitanufaika na mradi huo wa maji na kwamba  umegharimu  zaidi ya shilingi milioni 300.

Taarifa ya mwandishi wetu Kale Chongela inafafanua zaidi.

Sauti ya ufafanuzi wa taarifa