Storm FM

Hizi hapa bei mpya za mafuta Geita kwa mwezi Septemba

3 September 2025, 9:53 am

Muonekano wa roundabout iliyopo mkoani Geita katika barabara ya makutano. Picha kutoka maktaba

Kila Jumatano ya kwanza ya kila mwezi mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji nchini (EWURA) hutangaza bei kikomo za mafuta ya Petroli, Dizeli na mafuta ya taa.

Na: Ester Mabula

Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji nchini EWURA imetangaza bei mpa kikomo za mafuta kwa mwezi Septemba, 2025.

Katika wilaya za Mkoa wa Geita bei mpya za mafuta ni kama ifuatavyo:

Wilaya ya Geita Petroli ni 3,007 kwa lita na Dizeli ni 2955

Wilaya ya Bukombe Petroli ni 2996 kwa lita na Dizeli ni 2944

Wilaya ya  Chato Petroli ni 3028 kwa lita na Dizeli ni 2976

Wilaya ya Mbogwe Petroli ni 3,045 kwa lita na Dizeli ni 2993

Wilaya ya Nyang’hwale Petroli ni 3,022 kwa lita na Dizeli ni 2970