Storm FM

Mahafali ya 13 Waja Spring Geita, DC asisitiza malezi

23 August 2025, 8:14 pm

Wahitimu wa darasa la saba Waja Spring wakiwa katika mahafali ya 13. Picha na Edga Rwenduru

Malezi bora ndiyo msingi wa mafanikio ya baadaye kwani mtoto anayekuzwa katika mazingira mazuri huwa na nafasi kubwa ya kutimiza ndoto zake.

Na Mrisho Sadick:

Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita Sakika Mohamed amewataka wazazi na walezi kuweka kipaumbele katika malezi na makuzi ya mtoto badala ya kujikita zaidi kwenye shughuli za kiuchumi pekee.

Akizungumza kwenye mahafali ya 13 ya shule ya msingi na awali ya Waja Spring Manispaa ya Geita Mkoani Geita leo Agosti 23,2025 Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza kuwa malezi bora ndiyo msingi wa mafanikio ya baadaye kwani mtoto anayekuzwa katika mazingira mazuri huwa na nafasi kubwa ya kufanikisha ndoto zake.

Mkuu wa wilaya ya Mbogwe akizungumza kwenye mahafali ya 13 ya Waja Spring. Picha na Edga Rwenduru

Kwa upande wake Mkurugenzi mwenza wa shule za Waja, Jacqueline Tesha amesema shule hiyo imekuwa na historia ya kufanya vizuri kitaaluma tangu kuanzishwa kwake nakwamba mafanikio hayo yanatokana na mshikamanio wa walimu, wazazi na wanafunzi, huku akiwasihi wazazi kuendelea kushirikiana ili shule iendelee kushika nafasi ya juu kielimu nakuwataka wazazi na walezi kuweka nguvu katika malezi.

Mkurugenzi mwenza wa shule za Waja Jacqueline Tesha akizungumza kwenye mahafali ya 13. Picha na Edga Rwenduru

Awali muhitimu wa darasa la saba Grace Alex akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake amesema wahitimu wa darasa la saba wako 85 , wavulana 40 na wasichana 45 nakwamba katika kipindi cha miaka saba wawapo shule wamekuwa na mafanikio makubwa hususani ya kitaaluma kwa kufanya vizuri katika mitihani ya ndani na nje ya shule hiyo huku akisisitiza malezi ndio msingi wa mafanikio kwa mtoto.

Sauti ya Ripoti kamili ya stori hii