Storm FM
Storm FM
19 August 2025, 4:04 pm

Hadi sasa tayari shilingi milioni 3 zimekusanywa kupitia jitihada za jamii na wadau mbalimbali, kati ya milioni 60 zinazohitajika
Na Mrisho Sadick:
Zahanati ya Buseresere Wilayani Chato inahitaji jumla ya shilingi milioni 60 ili kukamilisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto lililodumu kwa zaidi ya miaka 14 bila kufanyiwa ukamilishaji.
Akizungumza katika mbio za hisani zilizolenga kuchangia ukamilishaji wa jengo hilo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Chato Thomas Dime amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kutenga fedha kupitia mapato ya ndani ili kuhakikisha ndoto ya wananchi wa eneo hilo inatimia.

Mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto, Ezron Yuda, pamoja na Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Buseresere, Edmundi Wilbad, wamesema wameanzisha mbio za hisani zilizojulikana kama Tuwavushe Mama na Mtoto Buseresere Marathonili kusaidia kufanikisha ujenzi huo na kuboresha huduma za afya ya uzazi na mtoto.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Dkt. Daniel Mzee amesema kutokana na udogo wa miundombinu ya zahanati hiyo, serikali imepanua huduma katika maeneo jirani ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mapinduzi ili kupunguza msongamano wa wagonjwa.