Storm FM

Wamiliki wa bar wanaoajiri watoto Sengerema waonywa

2 July 2025, 12:00 pm

Picha kutoka mtandanoni kupitia kwa Gsengoblog

Kushamiri kwa vitendo vya watoto wadogo kutumikishwa kwenye shughuli za bar imewaibua wananchi Sengerema

Na Emmanuel Twimanye:

Wamiliki wa bar katika kata ya misheni Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza wamepigwa marufuku kuajiri watoto chini ya umri wa miaka 18 kwa kuwa ni kinyume cha sheria.

Marufuku hiyo imetolewa na Askari  polisi kata ya Misheni  Insipekta  Asha Mohamed wakati akitoa elimu ya masuala ya ulinzi na usalama mahala pakazi  kwa wamiliki wa baa  katika kata hiyo.

Katika hatua nyingine  amewaonya wahudumu wa baa kuacha mara moja tabia ya kugonganisha wanaume ili kuepuka uvunjifu wa amani.

Sauti ya mkaguzi wa polisi

Viongozi wa Serikali ya mtaa na polisi jamii kata ya Misheni wameahidi kufanya msako mkali sehemu za baa ili kukokomesha ajira hatarishi kwa watoto.

Sauti ya viongozi wa serikali ya mtaa na polisi jamii

 Baadhi ya wamiliki wa baa wameahidi kutekeleza suala hilo ili kufanya kazi katika mazingira rafiki.

Sauti ya wamiliki wa bar na wananchi