Storm FM

Waliokosa mkopo wa 10% waandamana Geita

20 May 2025, 4:17 pm

Baadhi ya wana vikundi waliokosa mkopo wakipewa maelezo na viongozi wa kata. Picha na Kale Chongela

Mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri imezua kizaa zaa baada ya baadhi ya watu kukosa katika halmashauri ya manispaa ya Geita.

Na: Kale Chongela:

Baadhi ya wananchi kata ya kalangalala, halmashauri ya manispaa ya Geita wamelalamikia kitendo cha kukosa mkopo wa fedha za asilimia kumi inayotolewa na halmashauri kupitia mapato ya ndani licha ya kutuma maombi na kutumia gharama zao ikiwemo kusajili vikundi.

Wakiwa katika ofisi ya kata ya Kalangalala baadhi ya viongozi na wanachama wa vikundi hivyo wamesema walipokea ujumbe wa wito kutoka kwa Afisa mandeleo ya Jamii wa kata hiyo kufika ofisni kwake kuchukua nyaraka zao na barua inayoeleza sababu za kukosa mikopo hiyo ya halmashauri.

Wana vikundi wakiwa katika ofisi za kata ya Kalangalala baada ya kuandamana. Picha na Kale Chongela
Sauti ya wananchi

Diwani wa kata ya Kalangalala Mhe. Prudence Temba ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi walioomba mikopo hiyo kuwa wavumilivu huku jitihada zikiendelea kufanyika za wao kupewa mikopo hiyo.

Sauti ya Diwani wa Kalangalala Prudence Temba

Malalamiko hayo yamefika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Geita ambapo ililazimika mkuu wa idara ya maendeleo ya Jamii manispaa ya Geita Ndugu Robert Sugura kuitwa ili kuweza kutoa ufafanuzi juu ya malalamiko hayo.

Sauti ya mkuu wa idara ya maendeleo manispaa ya Geita