Storm FM

Community policing outreach yahitimishwa Nyarugusu

17 April 2025, 10:49 am

Kamishna wa Polisi Jamii nchini Tanzania Faustine Shilogile akizungumza na wananchi (hawapo pichani)

April 16, 2025 mkoa wa Geita kupitia Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na GGML umehitimisha program iliyokuwa na lengo la kutoa elimu kwa Jamii juu ya kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

Na: Ester Mabula:

Programu ya kutoa elimu kwa jamii juu ya kukabiliana na uhalifu, iliyokuwa ikiendeshwa na Jeshi la Polisi kupitia Kamisheni ya Polisi Jamii kwa ufadhili wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), imehitimishwa rasmi kwa mafanikio makubwa.

Wafanyakazi wa GGML wakiwa katika hafla ya kufunga program ya utoaji. Picha na Ester Mabula

Mpango huu ambao ulikuwa na lengo la kuongeza uelewa wa wananchi juu ya mbinu bora za kujilinda na kushirikiana na vyombo vya dola katika kupambana na uhalifu, umefikia tamati baada ya kufanyika kwa mfululizo wa warsha, mikutano ya hadhara na vipindi vya uelimishaji katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Geita.

Akizungumza katika hafla ya kufunga programu hiyo, Kamishna wa Polisi Jamii nchini Faustine Shilogile ameeleza mafanikio yaliyopatikana ni ushahidi wa nguvu ya ushirikiano kati ya vyombo vya dola na wadau wa maendeleo pamoja na wananchi katika kuimarisha usalama wa wananchi.

Sauti ya Kamishna wa polisi Jamii Faustine Shilogile

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa baadhi ya watu hususani viongozi wa dini wanaojihusisha na vitendo vya ukatili.

Sauti ya Kamishna wa polisi Jamii Faustine Shilogile
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akizungumza na wananchi. Picha na Ester Mabula

Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo ametoa shukrani kwa GGML kuweza kufanikisha program hiyo na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Polisi Jamii ili kufichua vitendo vya uhalifu

Sauti ya kamanda wa polisi Geita SACP Safia Jongo

Programu hii imekuwa mfano bora wa jinsi ushirikiano kati ya sekta binafsi na vyombo vya usalama unavyoweza kuleta mabadiliko chanya katika jamii, hasa katika maeneo yenye changamoto ya kiusalama.

Wananchi mbalimbali wakiwa katika hafla ya kuhitimisha program ya utoaji elimu. Picha na Ester Mabula