Storm FM

CCM wilaya ya Geita yaridhishwa na huduma kituo cha Nyarugusu

7 April 2025, 11:49 am

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita Barnabas Mapande akisalimiana na wajumbe wa Jumuiya ya wazazi

“Serikali inayo dhamira ya dhati ya kuhakikisha huduma za Afya zinakuwa bora kwa kila mwananchi” – Barnabas Mapande

Na: Kale Chongela:

Serikali imenunua vifaa tiba vya kisasa na kuongeza madaktari kwenye Kituo cha Afya Nyarugusu wilayani Geita kinachohudumia zaidi ya kata tatu ili kuwaondolea changamoto wananchi ya kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 38 kufuata huduma hizo hospitali ya wilaya.

Akitoa taarifa ya Kituo hicho mbele ya Jumuiya ya wazazi ya CCM wilaya ya Geita iliyotembelea katika kituo hicho ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya wazazi, Kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho Dkt Fedrick Felician amesema serikali imewapatia vifaa vya kisasa ikiwemo mashine ya Utra sound, mashine ya kinywa na meno ambazo zimekuwa msaada kwa wananchi wa eneo hilo.

Muonekano wa mashine ya Utra sound ambayo imenunuliwa na serikali. Picha na Kale Chongela

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Geita Robert Nyamaigolo na Katibu wa malezi na mazingira wa Jumuiya hiyo Paschal Mapung’o wameipongeza serikali kwa hatua hiyo kwakuwa Kituo hicho kinahudumia watu zaidi ya Elfu 70.

Sauti ya mwenyekiti na katibu wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Geita

Baadhi ya wanawake ambao tayari wamepata huduma katika kituo hicho wametumia fursa hiyo kuipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuwajali wananchi sambamba na kupongeza utoaji wa huduma katika kituo hicho.

Sauti ya wanawake

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita Barnabas Mapande amewataka watumishi wa kituo hicho kutumia vifaa hivyo kuwasaidia wananchi kwa kuwa ndiyo dhamira ya serikali.

Sauti ya mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita Barnabas Mapande
Muonekano wa ubao uliopo katika kituo cha Afya Nyarugusu. Picha na Kale Chongela