Storm FM

Ugawaji vibanda vya biashara Nyankumbu wazua balaa

24 March 2025, 3:11 pm

Muonekano wa vibanda vya baishara katika soko la asubuhi Nyankumbu.

Wajasiriamali waliopo katika soko la asubuhi Nyankumbu kata ya Nyankumbu, katika halmashauri ya manispaa ya Geita wamedai kutoridhishwa na utaratibu unaofanyika wa ugawaji wa maeneo ya kuuzia bidhaa.

Na: Kale Chongela – Geita

Wakizungumza na Storm FM leo Machi 24, 2025 wamesema kuwa jambo hilo limeibuka mara baada ya baadhi ya wajasiriamali kukosa maeneo licha ya kufuata utaratibu uliowekwa ikiwemo kulipia eneo ambalo wanatakiwa kufanyia biashara.

Sauti ya wafanyabiashara

Mmoja wa wajasiriamali aliyepata kibanda katika eneo amesema waliopata ni wale ambao tayari wamefanya malipo kiasi cha shilingi elfu 45 kwa miezi mitatu.

Sauti ya mfanyabiashara aliyepata kibanda
Shughuli mbalimbali zikiendelea katika soko la asubuhi lililopo Nyankumbu

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wadogo wilaya ya Geita amepongeza uwepo wa vibanda hivyo na kueleza kuwa changamoto mbalimbali zilizobainika katika ugawaji vibanda zinaendelea kutatuliwa.

Sauti ya mwenyekiti wa wafanyabiashara wadogo

Mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Geita Yefred Myenzi akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu amesema kuwa taarifa alizonazo ni kwamba zoezi linaendelea vizuri na kwamba hajapokea malalamiko juu ya suala hilo.

Sauti ya mkurugenzi Yefred Myenzi
Shughuli mbalimbali zikiendelea katika soko la asubuhi lililopo Nyankumbu