Storm FM

Wawili mbaroni kwa ubakaji wa mwanafunzi (10), yumo mwalimu

20 March 2025, 12:13 pm

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa. Picha kwa hisani ya mtandao

Katika hali ya kushangaza mwanafunzi wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 10 amekuwa akifanyiwa vitendo vya ubakaji kwa zaidi ya mwezi mmoja na watu wawili akiwemo mwalimu wake.

Na: Emmanuel Twimanye – Sengerema

Jeshi la Polisi wilayani Sengerema mkoani Mwanza linawashikilia watu wawili  akiwemo mwalimu wa shule ya msingi Daud  Ochieng (37)  na  Adon Sospeter (53) wakazi wa kata ya Ibisabageni kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi (10) wa shule ya msingi Bukala Wilayani Sengerema kwa nyakati tofauti.

Akizungumzia tukio hilo mtoto aliyedaiwa kubakwa akiwa amelazwa katika hospitali teule ya wilaya ya Sengerema amekiri kubakwa na watu hao kwa nyakati tofauti .

Sauti ya mtoto

Mama mzazi wa mtoto huyo amesikitishwa na tukio hilo na kueleza kuwa baada ya kugundua afya ya mtoto wake imedhoofika  ndipo aliamua kumpeleka hospitalini kwa ajili ya uchunguzi huku akitupa lawama kwa watuhumiwa hao.

Sauti ya mama mzazi wa mtoto

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Mwanza Wibroad Mutafungwa amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa wote wawili na wapo mahabusu katika kituo cha Polisi wilayani Sengerema na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo kukamilika.

Sauti ya kamanda wa polisi Wilbroad Mutafungwa