Storm FM
Storm FM
8 March 2025, 11:49 am

Licha ya jitihada zinazofanywa na uongozi wa manispaa ya Geita wa kuweka mazingira safi na salama, bado baadhi ya wananchi wameendeleza tabia ya utupaji taka kiholela katika mazingira yasio rasmi.
Na: Kale Chongela – Geita
Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Elimu kata ya Nyankumbu Manispaa ya Geita wamelalamikia changamoto ya baadhi ya wananchi kutupa taka ngumu katika eneo ambalo lipo wazi hali inayopelekea uchafuzi wa mazingira
Hayo yameelezwa Marchi 07, 2025 na baadhi ya wananchi wa eneo hilo ambapo wamebainisha kuwa licha ya eneo hilo kuwa katikati ya makazi ya watu wamekuwa wakikuta taka hizo zimetupwa na kueleza kuwa watu hao wamekuwa wakitupa nyakati za usiku.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw. Hassan Mshora amekiri kuwepo kwa hali hiyo na kueleza kuwa wanatarajia kuanza kufanya ulinzi katika eneo hilo ili kubaini wanaotupa taka ngumu katika eneo hilo.
Hata hivyo, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Geita Yefred Myenzi amesema wana mpango wa kuwanyang’anya maeneo watu wambao wametelekeza maeneo yao na kutoyaendeleza jambo ambalo linapelekea baadhi ya watu kuyatumia kwa kutupa taka.
