Storm FM

Wachimbaji waomba mgodi uliofungwa ufunguliwe Mbogwe

26 September 2024, 4:14 am

Baadhi ya wananchi wa kata Nyakafuru wakiwa katika mkutano wa hadhara wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela. Picha na Edga Rwenduru

Baadhi ya wananchi mkoani Geita wamekuwa wakijihusisha na shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu ili kuendesha maisha yao pamoja na kupata kipato cha kumudu gharama za maisha.

Na: Edga Rwenduru -Geita

Wachimbaji wadogo katika mgodi wa Isanjabhadugu (maarufu Area B) uliopo kata ya Nyakafuru wilayani Mbogwe mkoani Geita wameiomba serikali kupitia ofisi ya mkoa wa Geita kuufungua mgodi huo ambao ulifungwa baada ya mpasuko uliotokea katika eneo hilo ambao ulikuwa unahatarisha maisha ya wachimbaji hao.

Sauti ya wachimbaji

Wametoa maombi hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela Septemba 23, 2024 katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.

Mmoja ya wachimbaji akiwasilisha hoja yake mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Geita. Picha na Edga Rwenduru

Baadhi ya viongozi akiwemo makamu mwenyekiti wa wachimbaji wa Isanjabhadugu, Sangundi Mpigahodi amesema eneo hilo halifai kwa uchimbaji na sio salama kwa maisha ya binadamu.

Sauti ya kiongozi

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela amemwagiza afisa madini wa mkoa wa kimadini Mbogwe, wamiliki wa leseni pamoja na wachimbaji kufanya kikao cha mapendekezo ili kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.

Sauti ya RC Shigela
Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Nyakafuru. Picha na Edga Rwenduru