Storm FM

Kampeni ya ‘Tuwaambie kabla hawajaharibiwa’ ilivyozinduliwa Geita

24 September 2024, 3:37 pm

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya kupinga ukatili. Picha na Kale Chongela

Imeelezwa matukio ya ukatili ikiwemo vitendo vya ubakaji yameongezeka mkoani Geita kwa mwaka 2024 kufikia 91 kutoka 71 mwaka 2023.

Na: Kale Chongela – Geita

Wananchi mkoani Geita wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano juu ya vitendo vya ukatili ikiwemo upakaji ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na  kamanda wa jeshi la polisi mkoani Geita kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi SACP Safia Jongo Septemba 22, 2024 akiwa katika shule ya msingi Uwanja kata ya Nyankumbu mjini Geita kwenye uzinduzi wa kampeni ya kupinga vitendo vya ukatili.

Sauti ya Kamanda Geita

Kamanda Jongo amesema kwa mwaka 2023 matukio ya ubakaji yalikuwa 71 ambapo mwaka huu 2024 yameongezeka na kufikia matukio 91.

Msimamizi wa masuala ya kijinsia kutoka shirika la Plan Internation mkoani Geita Bi. Hildegada Mashauri amesema kila mmoja analo jukumu ya kumlinda mtoto ili atimize ndoto zake.

Sauti ya Hildegada Mashauri

Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela ambaye alikuwa mgeni rasmi ametumia fursa hiyo kuwataka wazazi na walezi kuwa makini na watoto wao juu ya matumizi ya simu kwani baadhi yao wanajifunza matendo yasiyofaa kupitia simu zao.

Sauti ya RC Geita
Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela akizungumza na wananchi kwenye uzinduzi wa kampeni ya kupinga ukatili.