Storm FM

Wakazi Nyakagomba wajengewa mnara wa mawasiliano

18 July 2024, 3:19 pm

Waziri Nape Nnauye akiwa kapanda juu ya mnara uliojengwa Nyakagomba. Picha na Edga Rwenduru

Serikali imejipanga kuboresha miundombinu ya mawasiliano itakaowezesha wananchi waishio maeneo ya vijijini kupata huduma ya mtandao.

Na: Edga Rwenduru – Geita

Wakazi wa kata ya Nyakagomba Halmashauri ya wilaya ya Geita Mkoani Geita wameondokana na changamoto ya muda mrefu ya ukosefu wa huduma ya mtandao baada ya serikali kutoa ruzuku ya ujenzi mnara wa mawasiliano ya simu katika eneo hilo.  

Wakazi wa kijiji cha Luhuha kata ya Nyakagomba wakimsikiliza waziri Nape Nnauye. Picha na Edga Rwenduru

Nzunga Solele, Zacharia Magesa na Masalu Marco ni wakazi wa kata hiyo ambapo wakizungumza wakati wa ziara ya waziri habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Nape Nnauye ya kukagua ujenzi wa mnara uliojengwa katika eneo hilo wamesema kabla ya ujenzi wa mnara huo walikuwa wanapanda mlimani kwaajili ya kupata huduma ya mtandao. 

Mbunge wa Busanda Mhandisi Tumaini Magesa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Geita mhe. Martine Shigela wamesema mnara huo umeghalimu zaidi ya shilingi milioni 100.

Sauti ya RC na mbunge
Waziri Nape Nnauye akizungumza na wananchi wa kijiji cha Luhuha. Picha na Edga Rwenduru

Waziri Nape Nauye amesema lengo la serikali ni kuhakikisha kila eneo linakuwa na huduma ya mtandao ili kurahisisha mawasiliano.