Storm FM

Mbunge wa Geita mjini atoa mitaji kwa wanawake 28

06/03/2026, 23:06

Mbunge wa Geita mjini Chacha Wambura akikabidhi mtaji kwa mmoja ya wanawake. Picha na Ester Mabula

Kaulimbiu ya maadhimisho ya siku ya wanawake kwa mwaka huu ni “Haki na Usawa kwa wanawake na wasichana: Msingi wa maendeleo Jumuishi kufikia Dira ya 2050”.

Na: Ester Mabula

Wanawake 28 mkoani Geita wamepatiwa mitaji ya kuendeleza biashara zao na Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Mhandisi Chacha Wambura.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Marchi 06, 2026 katika ukumbi wa Gedeco uliopo manispaa ya Geita mkoani Geita kwenye kongamano la wanawake lililoandaliwa na Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani.

Awali kabla ya kukabidhi mitaji hiyo Mbunge wa Geita mjini Mhe. Chacha Wambura ambaye alikuwa mgeni rasmi amewataka wanawake kuondoa dhana ya utegemezi na badala yake wajihusishe katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Sauti ya mbunge Geita mjini Chacha Wambura
Mbunge wa Jimbo la Geita mjini Mhandisi Chacha Wambura akizungumza na wanawake (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Naye Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Geita Regina Mikenze amesema kwa sasa Rais Samia Suluhu ametoa mikopo kwa wanawake kwa mtu mmoja mmoja na kuwaomba wanawake wachangamkie fursa hiyo ili wajikwamue kiuchumi

Sauti ya mbunge viti maalumu Regina Mikenze
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Geita Mhe. Regina Mikenze akizungumza na wanawake (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Aizungumza Afisa maendeleo ya Jamii mkoa wa Geita Bi. Martha Kaloso amewaomba wanawake kujitokeza kwa wingi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Marchi 08, 2026 ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Geita.

Sauti ya Afisa maendeleo ya Jamii Bi. Martha Kaloso

Wakizungumza  baadhi ya wanawake waliopatiwa mitaji hiyo Bi. Aziza Hassan na Suzana Thomas wamemshukuru Mbunge kwa kuwawezesha mitaji huku wakiahidi kuitumia kwaajili ya kuendeleza biashara zao.

Sauti ya wanawake