Storm FM
Storm FM
25 February 2026, 12:15 pm

“Naamini baada ya mafunzo haya mtaendelea kuwa na utendaji wenye tija na kuzingatia miiko ya utumishi wa UMMA kwa kujiepusha na vitendo vyenye kujenga taswira mbaya ya Serikali kwenye Jamii” -Mkurugenzi Yefred Myenzi
Na: Ester Mabula
Jumla ya watumishi 209 kutoka kada mbalimbali ambao ni waajiriwa wapya halmashauri ya manispaa ya Geita wamepewa mafunzo ya siku 2 yaliyofanyika Februari 23 – 24, 2026 ambayo yalilenga kuwajengea uwezo kwa kuwapatia maarifa na ujuzi utakaowasaidia kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi.
Akihitimisha mafunzo hayo jana Februari 24, 2026, Mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Geita Ndg. Yefred Myenzi amewaasa watumishi hao kuzingatia miiko ya utumishi na kuachana na vitendo vyenye kujenga taswira mbaya ya Serikali kwenye Jamii.

Kaimu mkuu wa idara ya utawala na usimamizi wa rasilimali watu Manispaa ya Geita Kadole Ngumungu, ametaja kada mbalimbali zilizopatiwa mafunzo sambamba na kutaja maeneo mahsusi yaliyofundishwa huku akieleza dhamira ya mafunzo hayo

Akizungumza mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Geita Said Lupunjaje aliyetoa mafunzo kwa watumishi hao amesema Taasisi hiyo itaendelea kutoa elimu kwa watu mbalimbali huku baadhi ya watumishi waliopewa mafunzo wakipongeza uwepo wa mafunzo hayo na kueleza namna watakavyo yatumia katika utendaji wao wa kazi.
