Storm FM

Lwamgasa Farmers Amcos waendesha harambee ununuzi wa trekta

18 February 2026, 1:28 pm

Mgeni rasmi, Diwani wa kata ya Lwamgasa Dkt. Daniel Mabala akizungumza. Picha na Kale Chogela

Chama cha ushirika kimekuwa na fursa mbalimbali ya kuwaunganisha wakulima katika kujadili na kufanya mambo ya kuleta tija kwenye kilimo.

Na: Kale Chongela

Chama cha ushirika cha Lwamgasa Farmers Amocos Limited kilichopo wilaya ya Geita mkoani Geita kimefanya harambe kwa  ajili ya kuchangisha fedha ili kununua  trekta na vifaa vya kilimo.

Diwani wa kata ya Lwamgasa Bw. Daniel Mabala akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye alitarajiwa kuwa  Naibu waziri TAMISEMI ofisi ya waziri mkuu anayeshughulikia afya Dkt. Jafari Rajabu Seif, amewapongeza wakulima kwa kuendelea kuonesha ushirikiano na kuhakikisha kila mkulima analima kilimo cha kisasa.

Sauti ya Diwani kata ya Lwamgasa, Daniel Mabala

Mwenyekiti wa Chama hicho cha ushirika Bw. Abdallah Rajabu ametumia fursa hiyo kuipongeza serikali ya awamu ya sita inayongoza na Dkt. Samia Suluhu kwa kutoa fedha ili kufanikisha upatikanaji wa mbegu na mbolea.  

Sauti ya mwenyekiti Abdallah Rajabu
Meneja wa chama cha Lwamgasa farmers Amcos akisoma risala mbele ya mgeni rasmi. Picha na Kale Chongela

Meneja wa chama hicho cha Ushirika  Ndugu Msafiri Makoye amesema chama hicho kimekuwa na mchango mkubwa kwa wakulimu huku akiwasihi wakulima wengine kujiunga na chama hicho.

Sauti ya Meneja, Msafiri Makoye
Baadhi ya wanachama wa chama cha ushirika Lwamgasa wakiwa katika harambee hiyo. Picha na Kale Chongela