Storm FM

Mbunge jimbo la Geita mjini aanza kutatuta kero ya barabara Buhalahala

15 February 2026, 11:38 am

“Nataka niseme kuanzia siku ya Jumanne, barabara zitaanza kufanyiwa matengenezo ili basi kero hii iweze kuondoka kwa wananchi wa eneo hili kwani serikali ya Rais Samia imetupa fedha kwaajili ya kukarabati miundombinu” – Mbunge Chacha Wambura

Na: Ester Mabula

Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Mhandisi Chacha Wambura amefanya ziara ya kukagua miundombinu ya elimu pamoja na barabara katika kata ya Buhalahala, ikiwa ni sehemu ya kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Katika ziara hiyo aliyoifanya Februari 14, 2026 ametembelea mitaa ya Kambarage, Michungwani na Nshinde ambapo awali aliweza kusikiliza kero za wananchi ambao wameeleza juu ya changamoto ya miundombinu ya barabara wakieleza kuwa wakati wa mvua barabara hizo hupitika kwa shida, hali inayochelewesha huduma za kijamii na kuathiri biashara.

Sauti ya wananchi
Mbunge wa Jimbo la Geita mjini Mhandisi Chacha Wambura akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Mbunge Chacha ameahidi kutatua kero hiyo ya miundombinu ya barabara katika maeneo aliyotembelea akisema zoezi la ukarabati litaanza Jumanne ya Februari 17, mwaka huu huku diwani wa kata ya Buhalahala Doto Nzanzui akimpongeza kwa kutenga muda wake na kuwafikia wananchi ili kukatua kero zao

Sauti ya mbunge na diwani kata ya Buhalahala

Katika ziara hiyo, Mbunge Chacha aliambatana na mhandisi Jerry Mwakapemba kutoka ofisi ya TARURA wilaya ya Geita ambaye alitoa maelezo kuhusu mpango wa ukarabati wa barabara hizo.

Sauti ya mhandisi kutoka ofisi ya TARURA
Jojina Samweli, mkazi wa kata ya Buhalahala akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya ubovu wa miundombinu. Picha na Ester Mabula