Storm FM

Akamatwa na kifaa cha kutengeneza noti bandia Geita

17 January 2026, 2:07 pm

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

“Jumla ya watuhumiwa 200 tumewakamata kwa makosa mbalimbali na tunaendelea na upelelezi zaidi ili kuwafikisha mahakamani” – SACP Safia Jongo

Na: Ester Mabula

Jeshi la polisi mkoa wa Geita limeendelea kuimarisha ulinzi na usalama wa mkoa kupitia oparesheni mbalimbali ambapo kwa kipindi cha kuanzia Januari mosi, 2026 hadi leo Januari 17, 2026 limefanikiwa kukamata jumla ya watuhumiwa 200 wa makosa mbalimbali.

Hayo yameelezwa leo Januari 17, 2026 na Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP) Safia Jongo wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo ameesema miongoni mwa wathumiwa waliokamatwa mtuhumiwa mmoja amekamatwa akiwa na mtambo wa kuchapisha noti bandia.

Sauti ya ripoti kamili na Ester Mabula
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akionesha noti bandia zilizokamatwa. Picha na Ester Mabula
Baadhi ya vitu ambavyo vimekamatwa katika oparesheni mbalimbali za polisi. Picha na Ester Mabula