Storm FM

Kijana akamatwa ugoni, wananchi wamtembezea kichapo

13 January 2026, 11:31 am

Wananchi na wakazi wa eneo hilo waliojitokeza kushuhudia tukio la fumanizi. Picha na Ester Mabula

“Wanawake watatumaliza, kwanini mtu asieleze kuwa kaolewa ili kuondoa matatizo yasiyo ya lazima” – Kijana aliyefumaniwa

Na: Ester Mabula

Kijana mmoja (jina limehifadhiwa) mwenye umri wa miaka 34 amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali, baada ya  kufumwa akiwa na mke wa mtu  chumbani katika eneo la  Bujora, Kata ya Mission, wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

‎Akizungumzia tukio hilo Januari 12, 2026, kijana huyo akiwa chini ya ulinzi wa polisi jamii amedai kuwa mwanamke huyo alimdanganya kuwa hajaolewa ambapo ndipo alianzisha nae mahusiano.

Sauti ya kijana aliyekamatwa ugoni

Mwanamke aliyekamatwa ugoni na kijana huyo (jina limehifadhiwa) amesema kuwa kilichopelekea hayo ni kutokana na mume wake kushindwa kuihudumia na kuitunza familia .

Sauti ya mwanamke aliyekamatwa ugoni

Akizungumzia tukio hilo, mume wa mwanamke huyo (jina limehifadhiwa) amedai kuwa hajawahi kuitelekeza familia yake na wala hana mke mwingine kama inavyoelezwa.

Sauti ya mume wa mwanamke aliyekamatwa ugoni

Wakizungumzia tukio hilo baadhi ya wakazi wa mtaa huo wamesikitishwa na tukio hilo na kuwaomba wanawake kuwa waaminifu kwenye ndoa zao.

Sauti ya wananchi

Kwa upande wake, Mwenyekiti  wa  mtaa wa  Mission Bw. Joseph Protas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuitaka jamii kuachana na vitendo hivyo ili kuepuka kuhatarisha maisha yao kwani baadhi ya wananchi kujawa jazba na kujichukulia sheria mkononi.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa Joseph Protas