Storm FM

Atia ngumu pikipiki kufungwa cheni kisa kitambulisho

8 January 2026, 12:40 pm

Mvutano kati ya Joseph Hamis aliyevaa koti jekundu na viongozi wa egesho lukilini. Picha na Kale Chongela

Hatua ya kufunga cheni inalenga kudhibiti waendesha pikipiki wanaojihusisha na shughuli za usafirishaji bila kuwa na vitambulisho.

Na Kale Chongela:

Uongozi wa egesho la pikipiki la Lukilini lililopo Mtaa wa Mkoani Kata ya Kalangalala Manispaa ya Geita umeanza kutekeleza agizo la Umoja wa Bodaboda Taifa linalowataka waendesha pikipiki wote kuwa na vitambulisho vya kazi vyenye taarifa zao muhimu ikiwa ni hatua ya kudhibiti vitendo vya uhalifu na kuimarisha usalama.

Utekelezaji wa agizo hilo umeibua mvutano baada ya pikipiki ya Joseph Hamis mkazi wa Kijiji cha Bugarama Halmashauri ya Wilaya ya Geita, kuzuia pikipiki yake kufungwa cheni katika egesho hilo kwa madai kuwa hana kitambulisho kinachomruhusu kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa taratibu zao.

Baadhi ya waendesha pikipiki na wananchi katika egesho la lukilini mtaa wa mkoani. Picha na Kale Chongela

Akizungumza kuhusu tukio hilo, msimamizi wa egesho la bodaboda eneo la Lukilini Kata ya Kalangalala  Bw. Siwema Saga amekiri kutokea kwa mvutano huo na kueleza kuwa hatua ya kufunga cheni inalenga kudhibiti waendesha pikipiki wanaojihusisha na shughuli za usafirishaji bila kuwa na vitambulisho halali ikiwa ni kinyume na agizo la umoja wa bodaboda Taifa.

Sauti ya msimamizi wa egesho
Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa wa Geita akizungumzia sakata la vitambulisho. Picha na Kale Chongela

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa Umoja wa Bodaboda Mkoa wa Geita Ndugu Fred Fidel amesisitiza kuwa agizo hilo ni la lazima kwa waendesha pikipiki wote huku akiwataka wasimamizi wa maegesho kutumia njia rafiki za staha na zenye kuelimisha katika utekelezaji wa ukamataji na ufungaji cheni kwa wanaokiuka taratibu, ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Sauti ya mwenyekiti wa Bodaboda mkoa wa Geita