Storm FM

Sagayika agusa wahitaji kata ya Kalangalala

5 January 2026, 3:42 pm

Diwani wa kata ya Kalangalala Reuben Sagayika (aliyeshika maiki) akizungumza mara baada ya kufika gereza la wilaya ya Geita. Picha na mpiga picha wetu

“Ibada njema ni yenye kukumbuka watu wenye uhitaji na kuweza kuwasaidia ili waweze kujisikia vizuri kama watu wengine” – Diwani Sagayika

Na: Ester Mabula

Diwani wa kata ya Kalangalala Mhe. Ruben Emmanuel Sagayika ameuanza vyema mwaka 2026 kwa kuwakumbuka wagonjwa, watoto yatima pamoja na wafungwa waliopo katika gereza la wilaya ya Geita kwa kuwapatia mahitaji mbalimbali.

Mahitaji hayo yalitolewa Disemba 31, 2025 ambapo akiwa katika hospitali ya halmashauri ya manispaa ya Geita ameeleza kuwa mbali na kuwagusa wagonjwa ataendelea kuwa mwakilishi wa kusemea changamoto mbalimbali ndani ya kata yake.

Sauti ya Diwani kata ya Kalangalala

Watumishi katika hospitali hiyo akiwemo mganga mfawidhi Dkt. Thomas Mafuru pamoja na baadhi ya wagonjwa wamemshukuru Diwani kwa kuweza kuwapatia kwa msaada huo.

Sauti ya watumishi wa hospitali pamoja na wagonjwa
Mkuu wa Gereza la wilaya ya Geita (kulia) Mrakibu wa polisi Jovin Bugwina akitoa shukrani baada ya kupokea mahitaji. Picha na mpiga picha wetu

Akiwa katika gereza la wilaya ya Geita amesema serikali ya awamu ya sita inatambua makundi mbalimbali ya wananchi katika jamii huku Mkuu wa Gereza la Geita Mrakibu wa polisi Jovin Bugwina akitoa wito kwa wadau wengine kufata nyayo za kiongozi huy

Katika hatua nyingine diwani Sagayika ametoa zawadi kwa watoto Yatima wanaolelewa katika kituo Cha moyo wa huruma ambapo msimamizi mkuu wa kituo hicho Sister Maria Lauda amemshukuru diwani kwa kuongeza tabasamu katika nyuso za watoto hao huku akiikumbusha Jamii kuendelea kuwasaidia kwani mahitaji ya watoto ni mengi.

Sauti ya mkuu wa kituo cha Moyo wa huruma
Viongozi wa kata ya Kalangalala wakiwa na mkuu wa kituo cha Moyo wa huruma Sister Maria Lauda. Picha na mpiga picha wetu