Storm FM

Wanasimba wazindua mnara wa kisasa Mpomvu

14 October 2025, 11:19 am

Mwenyekiti tawi la Simba mtaa wa Mpomvu Bw. Yohane Mathias akizungumza na mwandishi wetu. (hayupo pichani). Picha na Edga Rwenduru

“Vilevile tunaendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa kushirikiana na serikali ikiwemo sekta za Afya na elimu” – Katibu wa tawi la Simba Mpomvu

Na: Edga Rwenduru

Mashabiki na wanachama wa klabu ya Simba katika mtaa wa Mpomvu uliopo kata ya Mtakuja halmashauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita wametumia kiasi cha shilingi milioni tatu kukamilisha ujenzi wa mnara wa kisasa katika tawi la klabu hiyo ambao umejengwa eneo la barabarani Mpomvu.

Akizungumza na Storm FM, mwenyekiti wa tawi hilo Bw.Yohane Mathias amesema tawi hilo lina zaidi ya wanachama 50 ambao wanakidhi vigezo huku wakiwa na nia ya kuendelea kuvuna wanachama wengi zaidi.

Sauti ya mwenyekiti Yohane Mathias

Aidha viongozi wa tawi hilo akiwemo Katibu wa tawi Masolwa Yombo wamesema tawi hilo pia linashiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kama kusaidia kwenye ujenzi wa zahanati na shule katika mtaa huo pamoja na kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Sauti ya katibu Masolwa Yombo
Muonekano wa mnara uliozinduliwa katika tawi la Mpomvu manispaa ya Geita. Picha na Edga Rwenduru

Baadhi ya mashabiki wa klabu hiyio waliyojitokeza katika uzinduzi wa mnara huo wamepongeza hatua hiyo na kueleza pia kufurahishwa na usajili wa klabu hiyo kwa msimu huu unaoendelea huku wakitarajia matokeo mazuri zaidi.

Sauti ya shabiki
Baadhi ya mashabiki wa klabu ya Simba waliojitokeza katika uzinduzi wa mnara. Picha na Edga Rwenduru